Tarehe 2 Juni, 2021
Huku watu wengi wakigeukia kupiga soga na biashara kwenye WhatsApp, leo katika F8 Refresh tunatangaza masasisho kwenye API ya WhatsApp Business, ambayo yatafanya iwe rahisi kwa biashara kuanza kutumia, na watu kupiga soga kwa urahisi na biashara hizo.
Tumepunguza muda ambao inachukua biashara kuanza kutumia kutoka wiki kadhaa hadi dakika tano tu. Iwe biashara inataka kufanya kazi na watoa huduma za biashara au kupata usaidizi wa moja kwa moja kutoka Facebook siku za usoni, uboreshaji huu utazirahisishia biashara za wastani na kubwa kuwa na mazungumzo na wateja kwenye WhatsApp.
Kwa vile biashara nyingi zinaingia katika WhatsApp, tunaboresha jinsi biashara zinavyoweza kuwasiliana na wateja wao. Kwa mfano, biashara zingeweza tu kutuma arifa kwa wakati, hali iliyofanya iwe vigumu kuwasiliana na wateja nje ya kipindi cha saa 24. Kwa hivyo sasa tutawezesha aina zaidi za mawasiliano -- kwa mfano, ili kuwajulisha watu wakati bidhaa iliyokwisha inapatikana tena. Pia tumeshuhudia jinsi arifa za mara kwa mara kutoka kwa mamlaka za afya kuhusu jinsi ya kukabili janga la sasa zimekuwa muhimu, na tunataka kufanya huduma kama hizo zipatikane kwenye aina nyingi za mawasiliano.
Pia tunaanzisha vipengele vipya vya utumaji ujumbe ambavyo vinaweza kuwasaidia watu kufanya biashara kwa haraka zaidi. Ujumbe mpya wa orodha unatoa menyu ya hadi machaguo 10 kwa hivyo si lazima tena watu waandike jibu. Vitufe vya kujibu vitawaruhusu watu kuchagua kwa urahisi miongoni mwa machaguo matatu kwa kubofya tu kile ambacho biashara zinaweza kuweka mapema kupitia akaunti zao za API ya WhatsApp Business.
Kama kawaida, watu wataendelea kudhibiti soga zao. Bado watu wanatakiwa kuanzisha mazungumzo au kuomba biashara ziwasiliane nao kupitia WhatsApp. Pamoja na masasisho haya, tunawapa watu njia mpya za kutoa maoni zaidi kuhusu hali yao ya utumiaji ilivyokuwa ikiwa wana sababu ya kuzuia biashara fulani.
Tunataka WhatsApp iwe njia bora na ya binafsi zaidi ya mawasiliano kati ya watu na biashara, tunafurahia sana hali hizi mpya tunazobuni ili kuboresha mawasiliano ya kibiashara.