Tarehe 21 Aprili 2023
Ukiwa na Jumbe Zinazotoweka mazungumzo sio lazima yadumu milele - kama tu mazungumzo ya ana kwa ana Ingawa safu hii ya ziada ya faragha hulinda jumbe dhidi ya kuendea wasiolengwa, wakati mwingine kuna ujumbe wa sauti wa mara kwa mara au sehemu kuu ya habari unayotaka kuhifadhi.
Leo tunaanzisha "Dumisha katika Gumzo," ili uweze kushikilia jumbe unazohitaji kwa ajili ya baadaye, kwa uwezo maalum wa kipekee kwa mtumaji. Tunaamini ikiwa umetuma ujumbe, ni chaguo lako ikiwa wengine kwenye gumzo wanaweza kuuhifadhi baadaye.
Ili kutimiza hili, mtumaji atajulishwa wakati mtu anahifadhi ujumbe, na mtumaji atakuwa na uwezo wa kupinga uamuzi huo. Ikiwa umeamua kwamba ujumbe wako hauwezi kuhifadhiwa na wengine, uamuzi wako ni wa mwisho, hakuna mtu mwingine anayeweza kuuhifadhi na ujumbe utafutwa wakati muda uliopimwa utakapoisha. Kwa njia hii una uamuzi wa mwisho kuhusu jinsi jumbe unazotuma zinalindwa.
Jumbe ambazo umehifadhi kwenye WhatsApp yako zitatambuliwa kwa aikoni ya alamisho na unaweza kuona jumbe hizi, zikipangwa kwa gumzo, kwenye folda ya Jumbe Zilizohifadhiwa.
Tunatumai watu watafurahia sasisho hili jipya na wepesi wa kuhifadhi jumbe wanazohitaji. Hii itaanzishwa kote ulimwenguni katika wiki chache zijazo.