Ukurasa Mkuu wa WhatsAppUkurasa Mkuu wa WhatsAppKushiriki Maono Yetu kuhusu Jumuiya kwenye WhatsApp
WHATSAPP WEB
VIPENGELE
PAKUA
USALAMA
KITUO CHA MSAADA

Chagua lugha yako

  • azərbaycan

  • Afrikaans

  • Bahasa Indonesia

  • Melayu

  • català

  • čeština

  • dansk

  • Deutsch

  • eesti

  • English

  • español

  • français

  • Gaeilge

  • hrvatski

  • italiano

  • Kiswahili

  • latviešu

  • lietuvių

  • magyar

  • Nederlands

  • norsk bokmål

  • o‘zbek

  • Filipino

  • polski

  • Português (Brasil)

  • Português (Portugal)

  • română

  • shqip

  • slovenčina

  • slovenščina

  • suomi

  • svenska

  • Tiếng Việt

  • Türkçe

  • Ελληνικά

  • български

  • қазақ тілі

  • македонски

  • русский

  • српски

  • українська

  • עברית

  • العربية

  • فارسی

  • اردو

  • বাংলা

  • हिन्दी

  • ગુજરાતી

  • ಕನ್ನಡ

  • मराठी

  • ਪੰਜਾਬੀ

  • தமிழ்

  • తెలుగు

  • മലയാളം

  • ไทย

  • 简体中文

  • 繁體中文(台灣)

  • 繁體中文(香港)

  • 日本語

  • 한국어

  • Pakua

  • Vipengele

  • Usalama

  • Kituo cha Msaada

  • Kuwa karibu

WhatsApp Blog

Kushiriki Maono Yetu kuhusu Jumuiya kwenye WhatsApp

Leo tuna furaha kushiriki maono yetu kuhusu kipengele kipya tunachoongeza kwenye WhatsApp kinachojulikana kama Jumuiya. Tangu tulipozindua WhatsApp mwaka wa 2009, lengo letu limekuwa kuwasaidia watu kuwasiliana kwa njia inayokaribiana na mazungumzo ya ana kwa ana wanapotaka kuzungumza na mtu binafsi, kikundi cha marafiki au familia. Pia, mara kwa mara tunapokea maoni kutoka kwa watu wanaotumia WhatsApp kuwasiliana na kuratibu shughuli katika jumuiya.

Mashirika kama vile shule, vikundi vya kieneo na mashirika yasiyo ya faida sasa yanatumia WhatsApp kuwasiliana kwa njia salama na kutekeleza mambo — hasa baada ya janga kutuchochea kutafuta njia za ubunifu za kufanya kazi pamoja tukiwa sehemu mbalimbali. Kutokana na maoni mengi ambayo tumepokea, tunaamini kuwa kuna mengi tunayoweza kufanya ili kuwawezesha watu kudhibiti mazungumzo haya yanayofanyika sana katika vikundi hivi.

Yote haya yatawezekana kupitia kipengele cha Jumuiya. Jumuiya kwenye WhatsApp zitawawezesha watu kuleta pamoja vikundi tofauti katika jumuiya moja inayowafaa. Kupitia hili, watu wanaweza kupokea taarifa zinazotumwa kwenye Jumuiya nzima na kupanga kwa urahisi vikundi vidogo vya kujadiliana kuhusu yaliyo muhimu kwao. Jumuiya pia zitajumuisha zana mpya mahiri kwa wasimamizi, ikiwemo kudhibiti vikundi vinavyoweza kujumuishwa, na ujumbe wa kutaarifu unaotumwa kwa watu wote.

Tunaamini kuwa Jumuiya zitamwezesha mwalimu mkuu wa shule kuwaleta pamoja wazazi wote wa shule ili kushiriki nao habari muhimu na kuanzisha vikundi vya madarasa mbalimbali, shughuli za ziada, au uhisani.

Pia tunafanya maboresho kadhaa kuhusu jinsi vikundi hufanya kazi kwenye WhatsApp — iwe vikundi hivyo ni sehemu ya Jumuiya au la. Tunaamini maboresho haya yatasaidia watu kushiriki maudhui kwa njia mpya na yatapunguza upakiaji wa soga nyingi mno katika vikundi vyenye washiriki wengi. Vipengele hivi vitapatikana katika wiki zijazo ili watu waanze kuvijaribu hata kabla ya Jumuiya kuwa tayari.

  • Maoni - Kipengele cha maoni ya emoji kitazinduliwa kwenye WhatsApp ili watu waweze kushiriki maoni yao kwa haraka bila kutuma ujumbe mpya kwenye soga.
  • Idhini ya Wasimamizi Kufuta Ujumbe - Wasimamizi wa vikundi wataweza kuondoa ujumbe usioruhusiwa au usiokubalika kwenye soga ya kila mtu.
  • Kushiriki Faili – Tunaongeza ukubwa wa faili unayoweza kushiriki hadi gigabaiti 2 ili watu waweze kushirikiana kwa urahisi katika miradi.
  • Simu za Kikundi Kikubwa – Tutazindua kipengele cha simu ya sauti chenye muundo mpya kinachoruhusu kupiga simu kwa hadi watu 32 kwa kugusa mara moja, wakati ambapo kuzungumza moja kwa moja kutafaa kuliko kupiga soga.

Mawasiliano kwenye jumuiya ni ya faragha, ndio maana tutaendelea kulinda ujumbe kupitia ufumbaji wa mwisho hadi mwisho. Teknolojia hii ya usalama ni muhimu sana katika kulinda faragha na usalama wa watu. Vikundi vya watu wanaoshirikiana kwa ukaribu — shule, washirika wa kanisa, hata wafanyabiashara — wangependa na wanahitaji kuwa na mazungumzo salama na ya faragha bila WhatsApp kufuatilia kila wanachokifanya. Unaweza kupata maelezo zaidi kuhusu jinsi tunavyoshughulikia faragha, usalama na ulinzi wa jumuiya hapa.

Ingawa programu zingine zinabuni njia za kupiga soga kwa ajili ya mamia ya maelfu ya watu, tunalenga kusaidia vikundi ambavyo ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Jumuiya kwenye WhatsApp ni huduma mpya hivyo lengo letu katika kipindi cha mwaka moja ujao ni kubuni vipengele vipya vitakavyotumika. Tunafuraha kuwaletea watumiaji huduma ya Jumuiya na tunatazamia kupokea maoni yao.

Aprili 14, 2022

MtwitoShiriki

WHATSAPP

Vipengele

Usalama

Pakua

WhatsApp Web

Biashara

Faragha

KAMPUNI

Kuhusu

Kazi

Kituo cha Bidhaa

Kuwa karibu

Blog

Hadithi za WhatsApp

PAKUA

Mac/PC

Android

iPhone

MSAADA

Kituo cha Msaada

Twitter

Facebook

Virusi vya Korona

2022 © WhatsApp LLC

Faragha na Masharti