Tarehe 6 Novemba, 2020
Kuanzia leo, watu kote nchini India wataweza kutuma pesa kupitia WhatsApp. Njia hii salama ya malipo inafanya shughuli ya kuhamisha pesa iwe rahisi tu kama kutuma ujumbe. Watu wanaweza kutuma pesa kwa familia zao kwa usalama au kuchangia gharama za bidhaa bila kubadilishana pesa taslimu kibinafsi au kwenda benki.
WhatsApp imeunda kipengele chetu cha malipo kwa kushirikiana na Shirika la Malipo la India (NPCI) kwa kutumia Kiolesura Unganifu cha Malipo (UPI), mfumo wa malipo kwa muda halisi ambao ni wa kwanza nchini India, unaowezesha miamala na zaidi ya benki 160 zilizowezeshwa. Tunafurahi kujiunga na harakati za India za kuongeza urahisi na utumiaji wa malipo dijitali, hali inayosaidia kukuza ujumuishaji wa kifedha nchini India.
Ili kutuma pesa kwenye WhatsApp nchini India, ni muhimu uwe na akaunti ya benki na kadi ya malipo nchini India. WhatsApp hutuma maagizo kwa benki, ambazo pia zinajulikana kama watoa huduma za malipo, ili kuanzisha uhamishaji wa pesa kupitia UPI kati ya akaunti ya benki ya mtumaji na ya mpokeaji. Ni fahari yetu kufanya kazi na benki tano zinazoongoza nchini India: ICICI Bank, HDFC Bank, Axis Bank, Benki ya Taifa ya India, na Jio Payments Bank. Watu wanaweza kutuma pesa kwenye WhatsApp kwa yeyote anayetumia programu ya UPI iliyowezeshwa.
Baada ya muda, tunaamini muungano wa usanifu wa kipekee wa WhatsApp na UPI unaweza kusaidi mashirika ya ndani kutatua baadhi ya changamoto muhimu za wakati wetu, ikiwa ni pamoja na kuongeza ushiriki wa vijijini kwenye uchumi wa kidijitali na uwasilishaji wa huduma za kifedha kwa wale ambao hawajawahi kuwa nazo.
Kama ilivyo kwa kila kipengele kwenye WhatsApp, mfumo wa malipo umeundwa na viunzi imara vya usalama na kanuni za faragha, ikiwa ni pamoja na hitaji la kuweka PIN ya UPI kwa kila malipo. Malipo kwenye WhatsApp yanapatikana kwa watu walio na toleo la hivi karibuni la programu za iPhone na Android.