Tarehe 15 Januari, 2021
Tumesikia kutoka kwa watu wengi jinsi ambavyo kuna mkanganyiko kuhusu sasisho letu la hivi karibuni. Kuna taarifa potofu zinazosababisha wasiwasi na tunataka kusaidia kila mmoja aelewe kanuni zetu na ukweli.
WhatsApp ilijengwa kwa kuzingatia wazo rahisi: unachoshiriki na familia na marafiki zako hukaa kati yenu. Hii ina maana kwamba huwa tunalinda mazungumzo yenu ya binafsi kwa ufumbaji wa mwisho hadi mwisho kila wakati, hivi kwamba WhatsApp wala Facebook haziwezi kuona ujumbe wenu wa faragha. Ndiyo maana hatuweki kumbukumbu ya watu wanaotumiwa ujumbe au kupigiwa simu. Pia hatuwezi kuona mahali unapopashiriki na hatuwezi kushiriki waasiliani wako na Facebook.
Kwa masasisho haya, hakuna hata moja inayobadilika. Badala yake, sasisho linajumuisha hiari mpyaambazo watu watakuwa nazo ili kutumia biashara ujumbe kwenye WhatsApp na linatoa uwazi zaidi kuhusu jinsi tunavyokusanya na kutumia data. Japo si kila mtu ananunua kutoka kwenye biashara inayotumia WhatsApp kwa sasa, tunadhani kwamba watu wengi watachagua kufanya hivyo siku za baadaye na ni muhimu watu wajue uwepo wa huduma hizi. Sasisho hili haliongezi uwezo wetu wa kushiriki data na Facebook.
Sasa tunasogeza mbele tarehe ambayo watu wataulizwa kuhakiki na kukubali masharti husika. Hakuna mtu atasitishiwa au kufutiwa akaunti yake tarehe 8 Februari. Tutaendeleza zaidi juhudi za kusahihisha taarifa potofu kuhusu jinsi faragha na usalama vinavyofanya kazi kwenye WhatsApp. Kisha tutawaendea watu taratibu ili waweze kuhakiki sera kwa mwendo wao wenyewe kabla ya kuanza kutumika kwa chaguo mpya za biashara tarehe 15 Mei.
WhatsApp ilisaidia kuleta ufumbaji wa mwisho hadi mwisho kwa watu kote duniani na tumejitolea kutetea teknolojia hii ya usalama sasa na baadaye. Shukrani kwa kila mmoja ambaye amewasiliana nasi na wengi ambao wamesaidia kusambaza ukweli na kukomesha uvumi. Tutaendelea kufanya kila tuwezalo ili kuboresha WhatsApp iwe njia bora ya kuwasiliana kwa faragha.